A Boys, vijana wawili ambao wanafanya vizuri katika sanaa ya muziki wa kizazi kipyan ndani na nje ya Zanzibar. “Basi Nipe Kidogo, Helelee. Aii Kidogo, Helelee” ni baadhi ya mashairi ya wimbo wa A Boys ‘Helele’ ambapo Harmonize alitajwa na yeye kahusika kusaidia kuandika mashairi ya wimbo huo.
Wakifanya mahojiano katika kipindi cha 5 Selekt cha EATV, “Ni Kweli kabisa, tunaweza kusema ni nyimbo kama mbili ambazo tumesaidiana na mdogo wetu Harmonize ambazo ni ‘Helele’ na ‘Nashukuru’” Alisema Jaco B.